Wana Lyrics

Hunywi maji yakapita
Mi nkigunu na ushafika
Jina gani hujaniita beiby

Ushauri hutaki kabisa
Eti uniache nina visa
Vya Firauni vya Musa vingi

Nikilala naota kama unaniita
Nafumba macho, navuta shuka
Naona napumbazika

Unishikapo ndipo hapo
Nafarijika
Mambo yako, mahaba yako
Ndo maana natononoka wee

Wana wana wana wana
Pale tulipokutana
Mikono tukapeana
Macho yakatizamana

Wana wana wana wana
Pale tulipokutana
Namba kubadilishana
Nafsi kukubaliana aah!

Nzi kidonda nimefia
Wahenga walisema
Maradhi yaweza yasiwe na dawa
Kwa penzi yakapona

Rabii, amenipa nusura
Jeuri sina tena
We ndo ganzi, umenimaliza hasira
Siumwi wakisema

Nidekeze, niliwaze
Washushuke wanyamaze
Nikuna nibembeleze
Usinipepee nipulize

Watume washituke
Roho zao ziwaume
Mi nipike ule chote
Unenepe upendeze

Wana wana wana wana
Pale tulipokutana
Mikono tukapeana
Macho yakatizamana

Wana wana wana wana
Pale tulipokutana
Namba kubadilishana
Nafsi kukubaliana aah!

Ukitaka uniweze nibebe wewe
Ukipenda unibimbe unikumbatie
Hata watu watuone wakahadithie
Nitambulishe niringe niwavimbie

Ukitaka uniweze nibebe wewe
Ukipenda unibimbe unikumbatie
Hata Lizer atuone wakahadithie
Nitambulishe nitambe niwavimbie

(Wasafi)


Related Lyrics

Added by

Zikitu

SHARE

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Search Artists