Daima Lyrics

Eric Wainaina-Daima

Umoja ni fahari yetu
Undugu ndio nguvu
Chuki na ukabila
Hatutaki hata kamwe
Lazima tuungane, tuijenge nchi yetu
Pasiwe hata mmoja
Anaetenganisha

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu

Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Kwa uchungu na mateso
Kwa vilio na huzuni
Tulinyakuliwa Uhuru
Na mashujaa wa zamani
Hawakushtushwa na risasi
Au kufungwa gerezani
Nia yao ukombozi
Kuvunja pingu za ukoloni

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu

Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Wajibu wetu
Ni Kuishi kwa upendo
Kutoka ziwa mpaka pwani
Kaskazini na kusini

Naishi, natumaini
Najitolea daima Kenya
Hakika ya bendera
Ni uthabiti wangu

Nyeusi ya wananchi na nyekundu ni ya damu
Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo

Kijani ni ya ardhi, nyeupe ya amani
Daima mimi mkenya
Mwananchi mzalendo


Related Lyrics

Added by

SHARE

VIDEO

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Search Artists